USIUZE KADI YAKO

USIUZE KADI YAKO

Focusradiotz

Jumatano, 14 Oktoba 2015

KITUO CHA MAWASILIANO CHA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI CHAZINULIWA



TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

 Mkurugenzi wa Uchaguzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi Ndug. Kailima Ramadhani na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP Bi. Awa Dabo, wakitoa taarifa fupi kuhusu kituo cha huduma kwa wapiga Kura.


 Mkurugenzi wa Uchaguzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi Ndug. Kailima Ramadhani na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP Bi. Awa Dabo, Kwa pamoja wakikata utepe kama ishara ya kuzindua kituo cha huduma kwa wapiga Kura.


KITUO CHA MAWASILIANO  CHA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Tume imeandaa kituo cha Mawasiliano “Call Center” kituo hiki kimeanzishwa ili kuweza kuwasaidia wadau wetu wa Uchaguzi hasa Wapiga kura kuweza kupata Elimu ya Mpiga Kura.

Wapiga kura wataweza kuuliza maswali mbalimbali yahusuyo Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani,
Ili kuweza kupata huduma hii unatakiwa kupiga namba 0800782100 bure na kuuliza maswali yako au kutoa taarifa yeyote kuhusu mwenendo wa Uchaguzi Mkuu.

Saa za Huduma
·      Kuanzia tarehe 12-18 Oktoba 2015 kituo kitafanya kazi kuanzia saa 2:00 Asubuhi hadi saa 12:00 Jioni
·      Kuanzia tarehe 19-30 Oktoba kituo kitafanya kazi kwa saa 24
Taarifa za simu zilizopokelewa kuanzia tarehe  Oktoba 12, 2015
Jumla simu 444 zilipokelewa tarehe 12/10/2015 na jumla simu 937 zilipokelewa tarehe 13/10/2015.


Tume inawaomba waandishi wa habari na wadau wengine kuisaidia Tume kutangaza namba hii 0800782100 ili wapiga kura waweze kupata taarifa mbalimbali.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni