USIUZE KADI YAKO

USIUZE KADI YAKO

Focusradiotz

Jumatano, 29 Julai 2015

DAFTARI LA AWALI LA WAPIGAKURA LAENDELEA KUCHAPISWA

 Mkurugenzi wa Uchaguzi mpya Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey usiku wa Tarehe 28/7/2015 akijionea hatua mbali mbali za uchapishaji wa Daftari la awali la wapigakura.
Tayari usambazaji katika mikoa sita umekwisha fanyika ikiwa ni Iringa, Mtwara, Njombe, Lindi, Rukwa na Mbeya kwa wananchi kuhakiki taarifa zao katika daftari la awali 'nataka hadi wiki ijayo tuwe tumebakiza Dar es Salaam tu sawa jamani, niambieni mapungufu yetu na asubuhi kesho tunayatatua kazi iende alisikika akiwaelekeza watendaji usiku ule hakuna kulala hapa kwa gharama yoyote alibainisha.
Taarifa za kuanza kwa uhakiki wa daftari la awali katika mikoa iliyosambaziwa zitatolewa punde katika mikoa husika kwa vyombo vya habari.Ni muhimu kuhakikisha Taarifa zako baada ya kujiandikisha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni