USIUZE KADI YAKO

USIUZE KADI YAKO

Focusradiotz

Jumatano, 29 Julai 2015

NEC YAKUTANA NA UONGOZI WA MKOA WA DAR ES SALAAM KUTATHIMINI ZOEZI ZIMA LA UANDIKISHWAJI BVR

 Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekutana na viongozi waandamizi wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiongozwa na mkuu wa mkoa huo, wakuu wa wilaya zote na wakurugenzi wa manispaa zote kutathimini hali ya zoezi zima la uandikishwaji mkoa wa Dar es salaam.

 Pamoja na changamoto zilizoainishwa ikiwemo rasimali Fedha yalijadiliwa kwakina,Tume imetoa wito kwa uongozi wa Dar es salaam kuhakikisha matatizo yaliyoainishwa yanatatuliwa katika siku zilizobaki ikiwemo uhaba wa watumishi vituoni suala la rushwa,na taarifa za mahitaji ya BVR kwa wakati kwani mashine hizo zipo za kutosha. 
  Serikali Pia imekwisha Toa madai yote ya kila mnispaa yaliyokuwa kikwazo katika zoezi zima linaloendelea mkoa wa Dar es Salaam ikiwemo rasilimali fedha. 

 Akiongea na waandishi wa Habari M/kiti wa Tume Jaji wa Rufaa mstaafu Damian Lubuva amesema hakuna mkazi yoyote hata andikishwa Dar Es salaam. Amewataka Wanahabari kuhakikisha wanakusanya taarifa sahihi kwa wakati na kuuelimisha umma wa Watanzania maswala yote yanayohusu Uandikishwaji na upigaji kura

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni